- Posted by Freebloggertemlatetz
- on
Claudia Wanjiru: Makovu yangu ndiyo urembo wangu, hayanizuii kuwa mwanamitindo
Claudia Wanjiru ni mwanamtindo
mwenye makovu usoni. Makovu hayo aliyapata baada ya kunusurika mkasa wa
moto akiwa mwanafunzi wa darasa la saba.
Kabla ya mkasa huo,
Claudia alikuwa na ndoto ya kuwa mwanamitindo, ndoto ambayo amehakikisha
ameitimiza licha ya kuwa na makovu usoni."Tulipokuwa kwenye hoteli tukiwekewa chakula, jiko la gesi lililipuka na mafuta yakanimwagikia usoni. Nilianza kukimbia nikitafuta maji".
Alichukuliwa kisha akapelekwa hospitalini. Alikuwa ameungua kwa asilimia kumi na nne usoni. Alikaa hospitalini kwa muda wa miezi mitatu. Hali hii ilifanya maisha yake kubadilika sana, hata kukosa marafiki.
"Baada ya kuungua, watoto ambao walikuwa wadogo kuniliko kwa umri, walikuwa wananiogopa, na wale ambao walikuwa wa rika langu, walikuwa wananicheka, wananitania. Nikiwa shuleni, nilikuwa napata barua za matusi na mwalimu akitupatia zoezi la kufanya kwa makundi, hakuna mtu alikuwa ananikubali tufanye naye pamoja," anasema.

Comments
Google+
To turn on Google+ comments:
Learn More